Jumatatu, 14 Machi 2016

WAKUU WAPYA WA MIKOA WATAAPISHWA KESHO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli amefanya uteuzi wa
wakuu wa mikoa 26 ya Tanzania
Bara ambapo kati yao 13 ni
wapya , 7 wamebakizwa katika
vituo vyao vya kazi, 5
wamehamishwa vituo vya kazi na
1 amepangiwa Mkoa Mpya wa
Songwe.
Uteuzi huo umetangazwa na
Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi
Mhandisi Mussa Ibrahim Iyombe
leo tarehe 13 March, 2016 Ikulu
Jijini Dar es salaam, wakuu wa
Mikoa walioteuliwa ni kama
ifuatavyo
1. Paul Makonda – Mkuu
wa Mkoa wa Dar es
salaam.
2. Meja Jenerali Mstaafu
Ezekiel Elias Kyunga –
Mkuu wa Mkoa wa Geita.
3. Meja Jenerali Mstaafu
Salum Mustafa Kijuu –
Mkuu wa Mkoa wa
Kagera.
4. Meja Jenerali Mstaafu
Raphael Muhuga – Mkuu
wa Mkoa wa Katavi.
5. Brigedia Jeneral Mstaafu
Emmanuel Maganga –
Mkuu wa Mkoa wa
Kigoma.
6. Godfrey Zambi – Mkuu
wa Mkoa wa Lindi.
7. Steven Kebwe – Mkuu wa
Mkoa wa Morogoro.
8. Kamishna Mstaafu wa
Polisi Zelote Steven –
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.
9. Anna Malecela Kilango –
Mkuu wa Mkoa wa
Shinyanga.
10. Mhandisi Methew
Mtigumwe – Mkuu wa
Mkoa wa Singida.
11. Antony Mataka – Mkuu
wa Mkoa wa Simiyu.
12. Aggrey Mwanri – Mkuu
wa Mkoa wa Tabora.
13. Martine Shigela – Mkuu
wa Mkoa wa Tanga.
14. Jordan Mungire
Rugimbana – Mkuu wa
Mkoa Dodoma.
15. Said Meck Sadick – Mkuu
wa Mkoa Kilimanjaro.
16. Magesa Mulongo – Mkuu
wa Mkoa Mara.
17. Amos Gabriel Makalla –
Mkuu wa Mkoa Mbeya.
18. John Vianey Mongella –
Mkuu wa Mkoa Mwanza.
19. Daudi Felix Ntibenda –
Mkuu wa Mkoa wa
Arusha.
20. Amina Juma Masenza –
Mkuu wa Mkoa wa Iringa.
21. Joel Nkaya Bendera –
Mkuu wa Mkoa wa
Manyara.
22. Halima Omary Dendegu
– Mkuu wa Mkoa wa
Mtwara.
23. Rehema Nchimbi – Mkuu
wa Mkoa wa Njombe.
24. Mhandisi Evarist Ndikilo
– Mkuu wa Mkoa wa
Pwani.
25. Said Thabit Mwambungu
– Mkuu wa Mkoa Ruvuma.
26. Luteni Mstaafu Chiku
Galawa – Mkuu wa Mkoa
wa Songwe (Mkoa mpya).
Kwa mujibu wa Kaimu Mkurugenzi
wa Mawasiliano IKULU Gerson
Msigwa, wakuu wote wa mikoa
walioteuliwa wataapishwa
Jumanne tarehe 15 March 2016
saa 3:30 Asubuhi Ikulu, Dar es
salaam.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni